Saturday 16 December 2017

Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 16.12.2017

Carlo Ancelotti atarudi Stamford Bridge na kuwa meneja wa Chelsea kabla ya kuanza kwa msimu mpya. (Daily Record)
Winga wa Monaco Thomas Lemar, 22, anawindwa na Chelsea, wanaotayarisha makubaliano ya fedha na mchezaji ya mshambuliaji Michy Batshuayi. (Daily Mirror)
Batshuayi, 24, anatarajia kuondoka Chelsea mwezi ujao kwa mkopo kupunguza hofu ya kupoteza nafasi yake katika kikosi cha Ubelgiji kitakachocheza katika kombe la dunia. (London Evening Standard)
Mchezaji kiungo cha kati raia wa Armenia Henrikh Mkhitaryan, 28, ametemwa na mkufunzi wa Manchester United, Jose Mourinho baada ya kuzuka mzozo kati yao wakati wa tathmini ya mechi katika uwanja wa mazoezi mwezi uliopita. (ESPN)
Mkufunzi huo wa ManUnited boss Mourinho ana nafasi ya kusajili wachezaji mwezi ujao, licha ya kwamba sio shabiki wa msimu wa usajili Januari. (Daily Mail)

0 comments: