Tuesday 26 December 2017

80% ya Ujenzi wa Barabara ya Manispaa ya Kinondoni kukamilika

Ujenzi wa barabara za awamu ya kwanza katika halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam kupitia Ufadhili wa Mradi wa Benki ya Dunia DMDP umekamilika kwa asilimia 80 huku kazi iliyobaki ikiwa ni ujenzi wa mitaro ya kupitisha maji ya mvua,Uwekaji taa za barabarani pamoja na njia za watembea kwa Miguu….

Akizungumza na Chanelten wakati wa Ukaguzi wa barabara hizo zinazounganisha Tanesco kuelekea Soko la Samaki Msasani, barabara ya viwandani eneo la Mwenge pamoja na barabara za Makumbusho, Mratibu wa Usimamizi wa mradi huo katika manispaa ya kinondoni Mkelewe Masalu Tungaraza amesema Mkandarasi aliyepewa kazi hiyo anatarajia kuIkamilisha Januari mwakani.

Kuhusu awamu ya pili ya Ujenzi wa barabara za Tandale,Maji Vhumvi -Kisukulu pamoja upanuzi na uwekaji kingo katika mto ng’ombe ili kupunguza athari za Mafuriko katika makazi ya wananchi amesema tayari Mkandarasi ameshapatikana na kazi imeanza,huku pia tathmini na malipo kwa wananchi ambao sehemu za nyumba zao zitavunjwa wanaendelea kulipwa fidia.

Mstahiki Meya wa Kinondoni Benjamini Sitta akizungumzia Umuhimu wa Miradi hiyo amesema itasaidia kupunguza foleni kwa wakazi wa msasani na maeneo yote ya makumbusho,lakini pia kupungua mafuriko ambayo imekuwa ikiwaathiri wakazi wa maeneo hayo pamoja na kuongeza thamani makazi yao.

0 comments: