Sunday 24 December 2017

Wanasayansi wa Anga wamegundua Nyota Mpya inayoendana na Jua

Shirika la anga za juu la Marekani maarufu kama NASA siku za hivi karibuni limegundua nyota ambayo inazungukwa na sayari nane, sawa na mfumo wetu wa jua ambao una sayari nane.
Inaelezwa kuwa hiyo ndiyo idadi ya juu zaidi ya sayari kugunduiwa zikiizunguka nyota nje ya mfumo wetu wa sayari. Nyota hiyo iliyopewa jina Kepler-90, ina joto kiasi na ni kubwa kidogo kulishinda Jua.
Hapo awali, wataalamu wa anga za juu waligundua uwepo wa sayari saba pekee zilizokuwa zinaizunguka lakini hivi karibuni wanasayansi wa Nasa wamegundua uwepo wa sayari nyingine ndogo iliyojaa mawe ambayo ndiyo inakamilisha idadi ya sayari hizo nane.

0 comments: