Tuesday 19 December 2017

Cyril Ramaphosa ndiye Kiongozi mpya wa chama cha ANC, Afrika Kusini

Ramposa ambaye alikuwa makamu wa rais wa chama hicho aliweza kumshinda mpinzani wake Nkosazana Dlamini-Zuma, ambaye ni waziri wa zamani na alikuwa mke wa rais Zuma kwa kura 2440 kwa 2161.
Kwa sasa Ramaphosa ameoneka kuwepo kwenye nafasi kubwa ya kuwa rais katika uchaguzi wa mwaka 2019.

Hata hivyo Cyril Ramposa amekuwa kiongozi wakati ambao Afrika kusini inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinafanya mambo hayendi sawa katika taifa hilo lenye uchumi mkubwa barani Afrika .
Cyril Ramaphosa ni mtu wa aina gani?
Cyril Ramposa alizaliwa tarehe 17 mwezi novemba mwaka 1952 mjini Soweto, ndio mwanasiasa tajiri zaidi Afrika Kusini ,utajiri wake unakisiwa kuwa ni dola milioni 450.Tangu ujana wake Ramposa alikuwa na ndoto ya kuwa mwanasiasa shupavu na hiyo ndio ilimfanya kujiunga na uongozi wa chama cha wafanyakazi, (BBC SWAHILI)

0 comments: