Wednesday 27 December 2017

Rwanda kupiga Kura juu ya Kanuni za Makosa ya Jinai

 Kigali, mji mkuu wa Rwanda

Wabunge nchini Rwanda wiki hii wataanza kupigia kura mswada mpya unaoeleza kanuni mpya za makosa ya jinai nchini humo.
Serikali, kupitia Tume ya Marekebisho ya Sheria ya Rwanda, ilianza kuchunguza kanuni mpya za makosa ya jinai za mwaka 2015 kama sehemu ya jitihada za kurejelea kuweka sawa mfumo sheria za makosa ya jinai nchini humo.
Serikali imekuwa ikibadilisha sheria hiyo tangu mwezi Oktoba mwaka huu.
Wizara ya Katiba na Sheria nchini humo inasema, lengo la mabadiliko hayo ni kufanya sheria hiyo kueleweka kwa urahisi na kukabiliana vilivyo na makosa mbalimbali.
Waziri wa Katiba ya SheriaEvode Uwizeyimana aliwaambia wabunge kwamba mabadiliko yaliyopendekezwa yanalenga kuifanya raihisi sheria ya makosa ya jinai katika kuitumia na nuifanya ngumu kwa kukomesha uhalifu, kuadhibu wale wote watakaopatikana na uhalifu huo na kukabiliana na wahalifu.
Katika mahojiano ya simu na gazeti la New Times jana Jumanne , Mbunge John Ruku-Rwabyoma alisema kama wabunge wenzake walikubaliana kuhusu ibara zote, Wanyarwanda watashuhudia mabadiliko mengi na watafurahi
Amebaini kwamba sheria kuhusu utoaji mimba, huenda ikakubaliwa na wabunge wenzake na, hii itakua ni hatua nzuri.

0 comments: