Thursday 21 December 2017

Kiwanda Cha Pombe Bandia Chanaswa Jijini Mwanza



Wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihimiza ulipaji wa kodi wapo wahujumu uchumi na wanaotumia vibaya Sera ya Tanzania ya viwanda.


Kupitia oparesheni iliyofanyika jana  usiku, Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limefanikiwa kubaini Kiwanda bubu cha pombe bandia  kilichokuwa kinazalisha pombe kali iliyopewa jina la 'kubumba'
Polisi wamekifunga kiwanda hicho na kumkamata mmiliki wake, Emanuel George Munisi maarufu kama CCM pamoja na wenzake wanne.

0 comments: