Sunday 24 December 2017

Liberia kupiga Kura 27.12.2017 katika Uchaguzi wa Rais Uliocheleweshwa

Waliberia watamchagua kiongozi mpya Jumanne (27.12.2017) katika uchaguzi wa duru ya pili kati ya makamu wa rais Joseph Boakai na mchezaji kandanda wa zamani maarufu George Weah.

Kura hiyo itaashiria mabadiliko  ya  kwanza  ya uongozi  nchini  humo  tangu  mwaka  1944.
Baada  ya  wiki  saba  za uchelewesho kutokana  na  malalamiko  ya kisheria  yaliyofikishwa  mahakamani  na  chama  tawala  cha Boakai  cha  Unity dhidi  ya  tume  ya  uchaguzi  nchini  humo, vituo vya  kupigia  kura  vinatarajiwa  kufunguliwa  kuanzia  saa  mbili asubuhi  saa  za  Liberia  na  kufungwa majira  ya  saa  12  jioni  kwa ajili  ya  wapigakura  milioni 2.1 waliandikishwa  kupiga  kura
Chama  cha  Weah cha  Muungano  kwa  ajili  ya  mabadiliko  ya kidemokrasi, Coalition for Democratic Change (CDC) kimewataka wapiga  kura  kutokunywa  pombe kupita  kiasi  katika  sikukuu  ya Krismasi na  kuamka  mapema  siku  ya  tarehe  26  kupiga  kura zao  katika  kile  mwenyekiti  wa  tume  ya  uchaguzi  ya  taifa  NEC, Francis Korkoya  alichosema  kuwa  ni "kujitolea  mhanga  kwa  ajili ya demokrasia  yetu  na  nchi  yetu."
Watachagua  mrithi  wa  rais Ellen Johnson Sirleaf, anayetarajiwa kuondoka  madarakani  mwezi  Januari  baada  ya  miaka  12 akiwa katika uongozi  wa  juu  wa  taifa  hilo  la  Afrika  Magharibi, linaloibuka  kutoka  katika  mavumbi  ya  vita  vya  wenyewe  kwa wenyewe,(1989-2003) na pia kushughulikia hatua za kupambana  na mzozo  wa  ugonjwa  wa  Ebola (2014-16).

DW SWAHILI.

0 comments: