Sunday 31 December 2017

Maandamano Makubwa nchini Irani.

Kumeshuhudiwa misururu mibaya ya ghasia kati ya waandamanaji na walinda usalama nchini Iran.

Mikanda ya video iliyowekwa katika mitandao ya kijamii, inaonesha, waandamanaji wawili wakipigwa risasi katika mji wa Dorud- Magharibi mwa taifa hilo.

Huko Ab-har, Kaskazini mwa taifa, waandamanaji waliteketeza bango kubwa iliyo na picha ya kiongozi mkuu wa kidini wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei.

Gari pamoja na pikipiki moja ya polisi, ziliteketezwa moto na waandamanaji huko Mashdad.


    Marekani yaiwekea Iran vikwazo



    Iran yawanyonga 'magaidi' 20



    Marekani yaiwekea Iran vikwazo



Katika mji mkuu Teh-ran, maelfu ya watu waliandamana hadi katika uwanja mmoja wa mkutano, ulioko katikati mwa mji huo, huku wakitoa wito kwa jeshi na polisi kuungana nao.

0 comments: