Sunday 17 December 2017

Makamu wa Rais wa Marekani Pence kwenda Mashariki ya kati.


Makamu  wa  rais  wa  Marekani  Mike Pence  atazuru  Jerusalem  siku  ya  Jumatano , akijitumbukiza   katika  mzozo  wa  moja  kati ya  suala  lenye  utata  kabisa   katika  mzozo kati  ya  Wapalestina  na  Israel.
Israel ilichukua  udhibiti  wa  sehemu  ya  mashariki  mwa  mji  huo  katika  vita  vya  mashariki ya  kati  mwaka  1967  na  inaliona  eneo  lote  la  mji  wa  Jerusalem  kuwa  mji  ambao haukugawanyika.

Wapalestina  wanaliona  eneo  la  mashariki  mwa  Jerusalem  kuwa  mji  mkuu  wao  wa hapo  baadaye.
Balozi  wa  Israel  katika  Umoja  wa  mataifa  Danny Danon "anashutumu  vikali" mswada huo , akipuuzia  kwamba  ni  juhudi za Wapalestina "kuandika  upya  historia."
"Hakuna  kura  ama  mjadala  utakaobadilisha  hali  halisi  kwamba Jerusalem ilikuwa  ama itakuwa  mji  mkuu  wa  Israel," danon  alisema  katika  taarifa.
Mswada  huo  wa  azimio  unatoa  wito kwa  nchi  zote kujizuwia  kufungua  balozi  zao   mjini Jerusalem, ukiakisi  wasi  wasi  kwamba  serikali  nyingine zinaweza  kufuata  kile  Marekani ilichofanya.

Mswada  huo  unataka  kwamba  mataifa  yote  wanachama  kutotambua  hatua  yoyote ambayo  itakwenda   kinyume  na  maazimio  ya  Umoja  wa  Mataifa  kuhusu  hadhi  ya  mji huo.
Maazimio  kadhaa  ya  Umoja  wa  mataifa  yanaitaka  Israel  kujiondoa  kutoka  katika  ardhi iliyokamata  wakati  wa  vita  vya  mwaka  1967 na  kusisitiza  haja  ya  kufikisha  mwisho kulikalia  eneo  la  Wapalestina. (DW SWAHILI)

0 comments: