Sunday 24 December 2017

Yanga yavuka Kizingiti na kufanikiwa kusonga mbele kombe la FA/ASFC

Klabu ya Soka ya Yanga imeweza kuibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi Reha FC inayoshiriki Ligi Daraja la Pili katika mchezo wa Kombe la Shirikisho la FA mzunguko wa pili mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Mchezo huo ambao timu ya Reha ilianza kwa kushambulia upande wa wapinzani wao na kuwashika vilivyo kwani hadi dakika 45 zinamalizika hakuna timu ailiyofunga katika kipindi cha pili timu ya Yanga ikabadilika na kuanza kujaribu kupiga mashuti ambapo dakika ya 82 mchezaji Pius Buswita aliwapatia Yanga bao la kwanza lilodumu kwa dakika tatu na Amiss Tambwe aliweza kuongeza bao lingine lilowafanya kusonga mbele katika michuano hiyo.

0 comments: