Thursday 21 December 2017

Catalonia kufanya Uchaguzi wake Mkuu leo

Raia wa Catalonia leo hii watachagua viongozi wao wapya, katika uchaguzi ambao serikali kuu ya Uhispania inaamini utamaliza msuguano wa kisiasa unaoendelea.
Serikali kuu ya Madrid iliuvunja utawala uliokuwepo awali, baada ya kuandaa kura ya maoni iliyodaiwa kutofuata kanuni, iliyotaka uhuru wa eneo hilo.
Rais wa Catalonia aliyeondolewa madarakani, Carles Puigdemont, amekuwa akiendeleza kampeni zake za kujitenga na Madrid akiwa uhamishoni nchini Ubelgiji kwa kupitia mitandao ya kijamii.

0 comments: