Friday 15 December 2017

HUYU HAPA Mbunge wa SIHA aliehama chama chake (CHADEMA) kilichompa Ubunge.

Hamahama ya wabunge wa vyama vya upinzani kwenda chama tawala cha Mapinduzi (CCM) zinaendelea kupamba moto kwa kasi, ambapo December 14, 2017  Mbunge wa Siha Kilimanjaro kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,  Dkt. Godwin Mollel ametangaza kujivua uanachama wa chama hicho na kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge wa Jimbo hilo.
“Nimeona nia ya dhati ya Serikali CCM kutetea rasirimali za Taifa, nikaona niweze kujiuzulu nafasi yangu ya ubunge ili niweze kwenda kujiunga kwa vitendo katika kulinda rasirimali za Taifa letu, aminini watu wangu wa Siha nimeona mbali katika maamuzi haya, wana CCM napendekeza na nyie mnipokee,” – Dkt Godwin Mollel

0 comments: