Saturday 16 December 2017

Serikali Kuwastaafisha Walimu wa UPE waliobaki Mashuleni.

Serikali ina mpango wa kuwastaafisha walimu wa UPE ambao bado wapo kazini.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka wizara ya elimu zinasema, serikali inaamua kuchukua uamuzi huo kutokana na walimu hao  kushindwa kuendana na mfumo wa elimu ambapo mitaaala ya siku hizi ni tofauti na ile ya zamani kama Vile matumizi ya teknolojia hivyo inawapa ugumu kwenye ufundishaji.

UPE (Universal Primary Education) ni mfumo  ambao ulianzishwa mwaka 1977 kwa lengo la  kurahisisha upatikanaji wa elimu hasa kwa watoto .Serikali ilichaguwa baadhi ya wahitimu darasa la saba la Mkoloni  na kupewa mafunzo ya ualimu ili wakafundishe shule za Msingi ,na ndio hawa tunaowaita walimu wa UPE.

0 comments: