Wednesday 17 January 2018

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO 17.01.2018



TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATANO 17.01.2018

Chelsea wamezungumza na West Ham kuhusu kumsajili Andy Carroll, 29, kwa mkataba wa kudumu. (Telegraph)

West Ham wapo tayari kusikiliza dau la kuanzia pauni milioni 20 ili kumuuza Andy Carroll. (Sky Sports)

Kiungo wa kimataifa wa Armenia Henrikh Mkitaryan, 28, anataka kuongezewa mshahara kwanza ili kuhama kutoka Manchester United kwenda Arsenal. (Mirror)

Alexis Sanchez alikuwa na wasiwasi na sera za kuchezesha kwa zamu za Pep Guardiola kabla Manchester City haijabadili mawazi ya kumsajili. (Manchester Evening News)

Zinedine Zidane amemtaka rais wa Real Madrid Florentino Perez kumsajili winga wa Manchester City Raheem Sterling kuziba pengo la Gareth Bale. (Don Balon)

Matumaini ya Real Madrid ya kumsajili Eden Hazard yanategenea iwapo Chelsea wataweza kumsajili Alexis Sanchez. (Don Balon)

Everton wanakaribia kumsajili winga wa Arsenal Theo Walcott, 28, siku ya Jumatano. (Liverpool Echo)

Mshambuliaji wa kimataifa wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 28, ameiomba Borussia Dortmund kumuachia ajiunge na Arsenal. (Mirror)

Baba yake Pierre-Emerick Aubameyang, ambaye pia ni wakala wake anasafiri kwenda London kuzungumza na Arsenal, kuhusu uhamisho wa mwanaye, huku Dortmund wakisubiri kuona kama wataweza kumpata Mitchy Batshuayi. (Bild)

Real Madrid wapo tayari kuapnda dau la euro milioni 70 kumsajili Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Dortmund. (Don Balon)

Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 26, ambaye mkataba wake unamalizika mwisho wa msimu lazima afanye vipimo vya afya na kukubali kukatwa mshahara kwa asilimia 20 kama anataka mkataba mpya Emirates. (Sun)

Juventus wanajiandaa kupanda dau la kumsajili beki wa kulia wa Arsenal Hector Bellerin. (Calciomercato)

Kiungo wa Liverpool Marko Grujic, 21, ananyatiwa na Middlesbrough na Cardiff City. (ESPN)

Aleix Vidal huenda akaondoka Barcelona na kuelekea EPL mwezi huu baada ya Sevilla kuacha kumfuatilia. (Estadio Deportivo)

Simon Mignolet anafikiria kuondoka Liverpool huku Napoli wakifikiria kupanda dau la euro milioni 20. (Het Niewsblad)

Chelsea wanataka kumsajili beki wa kushoto wa Roma Emerson Palmieri mwezi huu. (Gianluca Di Marzio)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anasisitiza kuwa Maroanne Fellaini lazima abakie Old Trafford. (Sun)

Mshambuliaji wa Southampton Manolo Gabbiadini, 26, huenda akarejea katika klabu yake ya zamani Bologna. (Sky Italia)

Tottenham ni miongoni mwa timu zinazomnyatia kiungo wa Norwich James Maddison, 21. (Evening Standard)

Barcelona wamekataa dau la pauni milioni 22.2 kutoka Inter Milan la kumtaka kiungo Rafinha, 24. Barca wanataka pauni milioni 35.5. (Mundo Deportivo)

Zinedine Zidane huenda akaondoka Real Madrid baada ya kupewa nafasi ya kuwa meneja wa timu ya taifa ya Ufaransa. (Diario Gol)

Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na siku njema

0 comments: