Wednesday 10 January 2018

Mwalimu wa shule ya msingi mwenye umri wa miaka 24 anashikiliwa na jeshi polisi baada ya kumuua kwa kumchoma kisu mume wake mwenye umri miaka 25 kwa madai ya kumyima tendo la ndoa nchini Uganda.

Harriet Nambi inasemekana amemuua Musa Batera kwa kukataa kushiriki naye tendo la ndoa kwa miezi miwili baada ya kujifungua kwa njia ya upasuaji.

Majirani zake wamesema, Nambi alikuwa analalamika kwamba mumewe ameshindwa kumtimizia  mahitaji yake ya ndoa licha ya yeye kumueleza mara nyingi kuwa anahitaji.

Nambi alitishia kumfanyia kitu kibaya mumewe ambaye ni dereva wa bodaboda na aliporejea nyumbani jioni ugomvi uliibuka na akachukua kisu na kumchoma hadi akafariki. Mwanaume huyo  ana wake wengine wawili.

Nambi amekamatwa na polisi wa Uganda na yupo kizuizini akisubiri mashtaka kuhusu mauaji. Mwili wa Batera ulikabidhiwa ndugu zake kwa mazishi.

0 comments: