Thursday 18 January 2018

Dar Young African SC Yashikwa Shati na Mwadui.


Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara klabu ya Yanga wamelazimishwa suluhu na Mwadui FC kwenye mchezo wa raundi ya 13 uliomalizika jioni hii uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Yanga chini ya kocha Mzambia George Lwandamina kwa mara ya kwanza tangu arudi kutoka kwao, imeshindwa kupata ushindi hivyo kubaki katika nafasi ya tano. Mwadui FC yenyewe imefikisha alama 13 na kupanda hadi nafasi ya 9.

Hii ni mechi ya pili Yanga inashindwa kupata ushindi ambapo mechi ya raundi ya 12 Disemba 2017, ilikubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Mbao FC ya Mwanza.

Yanga imefikisha alama 22 hivyo kushindwa kuifikia Mtibwa Sugar yenye alama 23 katika nafasi ya nne baada ya wikiendi iliyopita kushinda mechi yake ya raundi ya 13 dhidi ya Lipuli FC.

Kesho kutakuwa na michezo miwili ambapo vinara wa ligi Simba SC watakuwa wenyeji wa Singida United wakati Azam FC inayoshika nafasi ya pili itakuwa ugeneini mjini Ruvuma kucheza na Majimaji FC.

0 comments: