Wednesday 17 January 2018

MAREKANI YASITISHA MSAADA WA FEDHA KWA WAPALESTINA.

Utawala wa Rais Donald wa Marekani umesitisha zaidi ya nusu ya fedha zake ilizokuwa ikizitoa kwa Shirika la Umoja wa Mataifa linalosaidia Wapalestina.

Marekani imesema itatuma kiasi cha dola milioni 60 ya malipo yake ya kwanza ya mwaka huu, lakini itazuia dola milioni 65 kwa kile ilichosema ''..kufikiria mustakabali ujao''.

Maafisa wa Marekani wamesema shirika hilo la Umoja wa Mataifa linahitaji kufanyiwa tena tathmini.

Washngton imekuwa ikitoa karibu asilimia 30 ya bajeti yake, kutoa huduma za afya, elimu na huduma za jamii.

Awali Rais Donald Trump alisema nchi yake itakata msaada iwapo Wapalestina wanapinga juhudi za amani na Israel.

Kwa upande wake Afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa amesema hatua hiyo ita haribu matokeo mazuri ya maelfu ya Wapalestina wasio na maisha bora yenye usalama.
Naye Afisa wa Palestina Wasel Abu Youssef amesema uamuzi huo unathibitisha kwamba Marekani inaendelea kuangamiza haki za Wapalestina.

Hata hivyo msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani amesema uamuzi huo haukukusudia kumuadhabisha yeyote yule.

Jumapili iliyopita Rais wa Wapalestina, Mahmoud Abbas alimshutumu Rais Trump na kwa kuvuruga juhudi za kupayikana kwa amani Mashariki ya kati, Amesema kwamba hatakubali mpango wowote wa amani kutoka Marekani baada ya nchi hiyo kuutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel.

Ameilaumu Israel kwa kuuweka penmbeni mkataba wa Oslo wa mwaka 1994, ambao ndio ulianzisha mpango huo wa kupatikana kwa amani.

0 comments: