Thursday 11 January 2018

Maandamano ya ghasia kupinga mfumuko wa bei yaendelea Tunisia

Kumekuwa na muendelezo wa siku tatu wa ghasia za maandamano nchini Tunisia katika mji mkuu wa Tunis na miji mingine ya nchi hiyo.

Polisi wamekuwa wakirusha mabomu ya machozi kwa kundi kubwa la watu ambao wamekuwa wakilalamikia juu ya mfumuko wa bei ambao unaathiri upatikanaji wa mahitaji muhimu.
Waziri mkuu , Youssef Chahed amelaani kwa kile alichokiita kuwa ni hakikubaliki kwa kuwepo kwa fujo za waandamanaji.

Kwa upande wao waandamanaji ,nao pia wametoa malalamiko yanayofanana juu ya polisi.
Maandamano ni juu ya bei kuwa ghali , wamepandisha, nadhani hii ni hali ngumu sana kubadilika , labda kama rais huyu tutamuondoa"
Wafanyabiashara wengi wamekamatwa na polisi na kuibiwa huku vyombo vya usalama wakiwa wamewekea mkazo kulinda majengo ya serikali.

Watu wapatao mia mbili wamefungwa mpaka sasa na huku kuna kuna mpango mwingine wa kuwepo kwa maandamano mengine makubwa hapo kesho.

0 comments: