Monday 15 January 2018

LOWASSA: Magufuli Aliniomba Nirudi CCM

Mjumbe wa kamati kuu ya chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, Edward Lowassa amefichua kuwa Rais John Magufuli alimuomba arejee chama tawala cha CCM wakati wa mazungumzo yao juma lililopita .

Katika taarifa iliyotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, kwa waandishi wa habari Lowassa ameeleza "ujumbe wa Rasi Magufuli ulikuwa kunishawishi kutaka nirejee CCM, suala ambalo sikukubaliana nalo na nilimueleza Rais ya kwamba uamuzi wangu wa kukihama chama hicho na kujiunga na CHADEMA haukuwa wa kubahatisha"

Wiki iliopita, kiongozi huyo wa upinzani nchini Tanzania, ambaye pia ni Waziri mkuu wa zamani, alikutana na Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli Ikulu na kumsifu sana kwa kazi anayoifanya.


 CHANZO: BBC SWAHILI

0 comments: