Wednesday 17 January 2018

Anthony Joshua Ampuuza Joseph Parker


Antony Joshua mwanamasumbwi nguli mtajika kwa sasa, amepuuilizilia mbali kwa kicheko cha mfa maji haishi kutapa tapa baada ya madai ya utumizi wa dawa za kuongeza nguvu yaliyotolewa na bondia mwenziwe Joseph Parker na kumbatiza jina la mfalme wa utumizi wa dawa za kuongeza nguvu.

Haya yanatukia kukitarajiwa pambano baina ya mabondia nguli na mashuhuri Joshua na Parker, pambano linalotarajiwa mwishoni mwa mwezi wa tatu mwaka huu, hii ni mara ya kwanza katika historia kwa mabondia hawa wenye uzito wa juu duniani kukutana nchini Uingereza.

Joshua ana umri wa miaka 28, akiwa na umri huo tayari anashikilia mikanda miwili ya IBF na WBA wakati bondia mwenziwe kutoka New Zealand Parker ni bingwa wa WBO.

Joshua anasema ameshasikia maneno mengi mabaya mno dhidi yangu kiasi hakuna jipya tena, ninajua rekodi zangu, ndiyo maana sijishughulishi na tambo zisizo na tija.
Joshua aliongeza kuwasema kuwa maneno ya kashfa yapo tele kwenye ndondi sasa kama ni jambo la kawaida hupaswi kuayatumia kama zana za kuuzia pambano.

Shutuma za Parker alizivurumisha wakati alipokuwa akihojiwa na redio moja nchini New Zealand baada ya kuthibitishwa kwa tarehe ya pambano.

Hata hivyo, wakati alipokuwa akizungumza na BBC redio 5 mapema wiki hii, Parker alikubali alizungumza maneno yasikyokuwa na maana yoyote, sidhani kama anauraibu huo.

Joshua ambaye anatuhumiwa , naye alipokuwa na mahojiano na BBC katika kipindi cha Graham Norton mwishoni mwa wiki iliyopita alimwita mpinzani wake mfalme wa pai.

Mabondia wote hawa wawili wanatarajiwa kupanda ulingoni kutetea rekodi ya kutopigwa, ikumbukwe kwamba michuano ya Olimpiki ya mwaka 2012 bondia Joshua alishinda michuano yote 20.
Kambi ya mpinzani wake Parker inajiandaa kwa kumpa mbinu za kushambulia kidevu dhaifu cha Joshua kwa kutumia mbinu ya Wladimir Klitschko mwaka jana kama ushahidi kabla Yoshua alipotetea hadhi yake tena kuwa bingwa wa dunia wa WBA katika uwanja wa Wembley.

Kama mara tatu niliumizwa ama kusita kwenye pambano anasema Joshua,wakati alipokuwa na mkutano na waandishi habari na kusema kuwa amejifunza kupitia matatizo na dhoruba na kujinasibu kuwa hakuna binaadamu yeyote ulimwenguni atakaye sitisha safari yangu.
Parker hajawahi kushindwa katika mapambano yake 24 ya kimataifa ulingoni yakiwemo 18 aliyoshinda kwa KO.Anavimba kwa kusema kuwa amekuwa akimuangalia Joshua kwa muda mrefu sana. Najua uwezo wake, na yeye ananijua pia. Naujua udhaifu wake naye anadhani anaujua udhaifu wangu

Naamini nitalenga kidevu chake na kumtoa kwenye pambano kwa KO.

0 comments: