Friday 12 January 2018

HISTORIA FUPI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

HISTORIA YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUTOKA 1963 - 1964.

Mnamo mwaka 1934 kilianzishwa chama cha AA “African Association, hichi kilifanya kazi ya kupinga ubaguzi dhidi ya watu wa Zanzibar na kutafuta haki ya wakulima hasa wa karafu, kazi hii waliifanya kupitia matamsha ya michezo na sanaa.
Mwaka 1939 jamii ya washirazi walianzisha chama chao “Shirazi Association” (SA) kwa madhaminio ya kulinda na kutetea haki za jamii ya wanashirazi.

Ilipofika miaka ya 1948 chama cha “African Association” kilibadilishwa jina na kuitwa “Zanzibar African Association” (ZAA). Baada ya mabadaliko haya, chama cha “Zanzibar Nationalist Party” kilianzishwa kikiwa kimebeba maslai mapana ya jamii wenye asili za kiarabu. Kuanzia hapa historia ya Zanzibar ilikuwa na mweleko tofauti.

Ilipowadia mwaka 1957 Zanzibar African Association (ZAA) na Shirazi Association (SA) viliunganisha nguvu na kuamua kuungana na kikazaliwa chama cha Afro Shirazi Party (ASP) na mwenyekiti wake wa kwanza alikuwa Sheikh Abeid Amani karume huku nafasi ya ukatibu mkuu wa chama akishikilia Sheikh Thabit Kombo.

Chama cha Zanzibar and Pemba People’s Party (ZPPP) kilizaliwa rasmi mwaka 1959 na waanzilishi wa chama hiki ni washirazi ambao hawakuridhia wala kukubali muunganiko wa ZAA na SA uliopelekea ASP kuzaliwa. Najaribu kukurudisha katika historia hii ili uwe na uelewa wa hii historia na chanzo cha mapinduzi ya Zanzibar.

Baada ya muunganiko na uwepo huo wa vyama hivyo vya siasa, mwaka 1961 mwezi wa kwanza kulifanyika uchaguzi wa vyama vingi, na vyama vilivyo shiriki uchaguzi vilikuwa ni ASP, ZPPP na ZNP. Baada ya uchaguzi hakuna chama kilichopata kura za kutosha kuanzisha serikali. ASP walipata viti 10, ZNP viti 9 wakati ZPPP walipata viti 3, ambapo baadaye walipoteza kiti kimoja kilicho enda ASP hivyo kukifanya kuwa na jumla ya viti 11, kwa hiyo jumla ya viti vya ZNP na ZPPP vilikuwa 11 dhidi ya 11 vya ASP, Hapa ukumbuke ZNP na ZPPP wanapigania kuunda serikali ya pamoja huku ASP kikisimama pekee yake.

Baada ya droo hiyo ya viti uchaguzi uliitishwa upya mwezi wa 6, 1961, awamu hii matokeo yalibalika ASP ikipata viti 10, ZNP viti 10 na ZPPP wakipata viti 3, hii ikaleta jumla ya kura 13 ya vyama viwili dhidi ya 10 ya chama cha ASP. Kwa matokeo hayo ZNP na ZPPP wakapata ridhaa ya kuunda serikali ya Zanzibar.

Uchaguzi mwingine ukafanyika mwezi wa 7,1963, safari hii viti vikaongezwa, matokeo yalipo tangazwa ASP walipata viti 13, ZPPP walipata viti 6, na ZNP wakapata viti 12, ikawapa jumla ya viti 19 dhidi ya viti 13 vya ASP hivyo ZNP na ZPPP wakaendelea kusalia madarakani kwa uhalali wa hayo matokeo.

Tarehe 10.12. 1963 Zanzibar ilitangazwa kuwa huru na Waingereza. Ikiwa chini ya Sultan Jeshmid bin Abdallah Al Said na waziri mkuu akawa Mohamed Shamte. Uhuru huu haukuwapendeza chama cha ASP ambapo wengi wa wanachama wake walikuwa waafrika wakati ule muungano wa ZNP na ZPPP wengi walikuwa ni waarabu, wazungu na wahindi. Hivyo iliaminika kuwa uhuru ule haukuwa kwa ajili ya wanyonge hasa wakulima katika mashamba ambapo kulikuwa na unyonywaji, ukandamizwaji, n.k. sababu nyingine za mapinduzi ni hujuma dhidi ya ASP katika chaguzi mbalimbali, waliona walikuwa na haki ya kushinda ila walikuwa wanahujumiwa.
Kutokana na kutoridhika huko waliamua kuunganisha nguvu zao kupitia vikundi mbalimbali, Vijana jasiri kama Seif Bakari, Kopa Omar (baba mzazi wa mwana muziki wa taarabu Khadija Kopa) na wanamapinduzi shupavu, akiwemo John Okelko, kuipindua serikali iliyokuwa madarakani.

 Mapinduzi haya yalifanyika na kufanikiwa kwa siku 33 tu toka uhuru wa mwezi wa 12 tarehe. 10, 1963.
Wakati wa mapinduzi Field Marshal John Okello kama alivyo jiiita, alisema “Mimi ni Field marshal Okello. Amkeni mabeberu, hapana tena serikali ya kibeberu, katika kisiwa hiki. Hivi sasa ipo serikali ya ipo serikali ya wapigania uhuru. Amkeni watu weusi. Kila mmoja wenu achukue bunduki au silaha nyingine na kupambana na mabaki ya mabeberu katika kisiwa hiki. Msichoke kama mnataka kisiwa hiki kuwa chenu”  Baadaye John Okello alitoroka Zanzibar ingawa iliishi Zanzibar tangia 1952.

Baada ya mapinduzi Sultani Jeshmid nae alitoroka Zanzibar kwenda Dar es salaam, ambapo kwa taarifa zisizo rasmi alikaa siku mbili na kwa msaada wa Nyerere alirudi kwao Uingereza ambapo anaishi mpaka leo. Huku Hayati Amani Abeid Karume akiwa rais wa kwanza wa Zanzibar.

#Siyo kwa umuhimu ; Kisiwa cha Zanzibar kilikuwa na mvuto na historia ya kipekee tangia karne ya 11, ikiwa na visiwa vikubwa viwili, Unguja na Pemba, na visiwa vingine vidogo vidogo takribani  20. Hivyo wageni wengi hasa waarabu, wahindi, wazungu n.k walifika Zenj wengi kupitia mwongozo wa upepo wa Monsoon. Walipo fika wengi waliamua kutorudi kwao, wakaanza kuoana na kuzaliana. Ndio maana hata leo wakazi walio wengi wa Zanzibar wana rangi zinazo shabihiana na asili ya watu hao wa nje. Wengi ni kama waarabu, wahindi n.k
Hongera Zanzibar kwa kutimiza miaka 54 ya mapinduzi.

0 comments: