Thursday 4 January 2018

Donald Trump alimhadaa Kim Jong-Un kuhusu kitufe cha nyuklia?

Rais wa Marekani Donald Trump alimtahadharisha Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un kwamba ana kibonyezo au kitufe cha nyuklia kikubwa kuliko chake kwenye meza yake.

Trump alisema hayo kwenye ujumbe kupitia Twitter. Lakini je, ni kweli?

Kulipua silaha za nyuklia ni shughuli yenye utaratibu mwingi, si rahisi vile kama tuseme kubadilisha vituo kwenye runinga.
Jambo la kushangaza ni kwamba nchini Marekani msamiati wake unahusisha biskuti na mpira wa kandanda.

Ingawa tamko la kuwepo "kitufe cha nyuklia" linafahamika sana, ukweli ni kwamba ni ufupisho wa shughuli ndefu.

Kwa hivyo, jibu liko wazi.

Katika uhalisia, Donald Trump hata kitufe chochote cha kufyatua au kurusha silaha za nyuklia.

Trump ana nini?

Mnamo 20 Januari mwaka jana, msaidizi wa rais wa kijeshi aliyekuwa amebeba mkoba wa ngozi alihudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Donald Trump alifika akiandamana na Rais Obama.

Baada ya Trump kuapishwa, msaidizi huyo - na mkoba wake - alihama na kwenda kwa Trump.

Mkoba huo hufahamika kama "mpira wa kandanda wa nyuklia".
Mkoba huo unahitajika kutoa idhini ya kurushwa kwa silaha za nyuklia za Marekani na - kwa nadharia - huwa hauondoki karibu na rais wa Marekani.

Agosti, mtaalamu mmoja aliambia CNN kwamba hata Trump anapokuwa anacheza gofu, mkoba huo huwa anaubeba kwenye kigari cha kusafirisha wachezaji uwanjani.

I
Mkoba huu una nini?

Ukapewa nafasi ya kuchungulia kuangalia nini huwa ndani ya mkoba huo ambao hufahamika kama mpira wa kandanda wa nyuklia, unaweza kusikitika.

Hamna kitufe chochote cha silaha za nyuklia.

Na pia hakuna saa yoyote, inayoashiria mwisho wa dunia au vita vya Armageddon.

0 comments: