Sunday 25 February 2018

Wajue kiundani wababe wakiarabu watakaokutana na SIMBA SC. Si wa mchezo mchezo

Kaskazini mashariki mwa Misri unapatikana mji wa Port Said. Mji wa Port Said una ukubwa wa kilometa 30 tu sawa na mile 19. Una idadi ya wa watu wasiopungua laki sita. Mji huu ulianzishwa mwaka 1859 wakati wa ujenzi wa mfereji wa Suez. Miaka 61 baada ya kuanzishwa Port Said mwaka 1920 klabu ya Al Masry ilianzishwa.  Klabu ya Al Masry inatumia uwanja wa Al Masry club stadium unaobeba mashabiki 17,000. Uwanja huu inasadikia ulisababisha kusimamishwa kwa ligi kuu Misri mwaka 2012 baada ya vurugu kutokea.
Klabu ya Al Masry inakutana uso kwa uso na klabu ya Simba katika kombe shirikisho. Klabu ya Simba imeweka makazi yake mashariki mwa Tanzania katika jiji la Dar es salaam. Simba ilianzishwa miaka 16 baada ya Al Masry kuanzishwa mnamo mwaka 1936.  Jiji la Dar Es salaam pia lipo kwenye ukanda wa pwani kama ililivyo kwa jiji la Port  Said ambapo klabu ya Al Masry inapatikana. Jiji la Dar es salaam hapo awali lilijulikana kama Mzizima yaani mji wa afya njema kutokana na hali nzuri ya vyakula hasa hasa shughuli ya uvuvi wa samaki.

Sultan Majid bin said aliamua kutengeneza mji wake ndani ya Mzizima akauita nyumba ya aman yaani Dar (Nyumba) Es saalam (Amani). Kumbe Dar es salam maana yake nyumba ya amani ambapo kinyume chake ni Dar al hard yaan nyumba ya vita. Hapa majiji mawili yanakutana Jiji La Porto lenye vitimbi vya migogoro hasa katika mfereji wa Suez, pamoja na Vurugu za uwanja wa Port Said na jiji la Dar Es Salaam linalosifika kwa utulivu na aman.
Klabu ya Al Masry inaongozwa na kocha mkuu Hossan Hassan ambaye pia aliwahi kuwa mchezaji nguli wa zamani wa taifa la Misri. Hossan Hassan alizaliwa mwaka 1966 katika jiji la Cairo katika eneo la Helwan ambalo rais wa zamani wa Misri Gamal Abdel Nasser alitangaza eneo hilo kuwa mji wa viwanda. Hossan Hassan ndiye mfungaji bora wa muda wote wa timu taifa ya Misri akiwa na magoli 69 kwenye michezo 169. Anatajwa kama mchezaji bora katika historia ya soka barani Afrika. Anakumbukwa sana kule nchini Uswisi kwa kuitandika klabu ya Celtic magoli manne kwenye mchezo mmoja akiwa na klabu ya Neuchatel Xamax kwenye michuano ya kombe la UEFA.
Pia aliwahi kuichezea klabu hiyo Al Masry kunako mwaka 2004 mpaka 2006. Mnamo mwaka 2008 alipewa kandarasi ya kuionoa klabu hiyo. Alitundika daruga akiwa na miaka 42.
 Awali ya yote ni watoe hofu mashabiki wa Simba ambao wanadhani Al Masry ni klabu kubwa kama akina Al Ahly au Zamalek. Klabu hii haijawahi kutwaa ubingwa ligi kuu Misri tokea ligi hiyo ianzishwe mwaka 1948. ila imejitahidi kumaliza  nafasi tatu za juu kwenye msimamao wa ligi mara sita tu. Licha ya kuwa haina mafanikio makubwa sana ligi kuu lakini ni klabu yenye mashabiki wengi sana nyuma ya al Ahly, Zamalek na Ismalia. Ilikuwa na mafanikio makubwa sana miaka ya 1921 mpaka 1989. Imetwaa kombe la sultan mara 3, kombe la Misri mara moja mwaka 1998, na kombe la shirikisho la Misri mara moja nayo ni mwaka 1992.
Pia imetwaa kombe la kanda ya mfereji wa Suez mara 17 kombe ambalo kwa sasa halipo tena na lilikuwa likijumuisha timu za majiji matatu tu. Kikubwa Heshima kubwa walio nayo ni kuwa imekosa kushiriki ligi kuu miaka miwili tu, walishuka daraja mwaka 1957 mpka 1959 baada ya mgogoro mkubwa kwenye mfereji wa Suez ambapo mapato ya klabu yalishuka na baadhi ya wachezaji kuondoka. Kiwango chao msimu huu sio cha kutisha sana kama cha kama moto walio nao vijana wa Manara. Kwanza wapo nafasi ya 4 kwenye msimamo wao wa ligi wakiwa na alama 42 baada ya michezo 23. Katika michezo kumi ya mwisho ya ligi wameshinda michezo mitano wametoka suluhu michezo mitatu na wamepoteza miwili.
 Nitoe tahadhari, hawa jamaa nao wana balaa lao, wanagawa vipigo kwa timu kubwa na vya magoli mengi. Mnamo tarehe 5 mwezi wa pili walitoa dozi ya magoli manne ugenini kwa klabu ya El Maqasa, wakaliza El Tanta magol sita kwa mbili,  wakaizibua El Nasri ugenini kwa magoli matatu kwa mawili. Pia wakaitandika Zamalek ugenini goli moja.
Katika klabu hii wachezaji wa kuogopwa ni A Bance mwenye mabao matano akiwa na umri miaka 33, pamoja na mshambuliaji Ahmed Gomaa mwenye magoli 11 akiwa na umri wa miaka 29,  Ahmed Sokri kiungo machachari na mkongwe mwenye magoli matano akiwa na umri wa miaka 30, mwingine ni pamoja na Islam Abou Slemma mwenye magoli matano. Ni hayo tu.

0 comments: