Saturday 17 March 2018

Hoja tatu kutoka kwa hotuba ya Mugabe


Chama cha National Patriotic Front, NPF, kilichoundwa na waliokuwa mawaziri wa Zanu PF kimemtangaza Rais wake.

Chama hicho kipya kimetangaza kuwa Brigedia mstaafu Ambrose Mutinhiri atakuwa Rais wake, hatua ambayo inaelezwa kuungwa mkono na Robert Mugabe.

Ijumaa juma lililopita, Mutinhiri alijiuzulu ubunge na ndani ya Zanu PF, akionyesha kutounga mkono kuondolewa kwa Mugabe madarakani.

Mkutano wa Mugabe wa kwanza na waandishi wa habari tangu aondoke madarakani inasemekana uliandaliwa na chama cha NPF ambacho kina matumaini ya kumuondoa

Mnangagwa kwenye kinyang'anyiro cha mwezi Agosti.

Kwa miezi kadhaa sasa imekuwa ikidhaniwa kuwa huenda Mugabe atarejea tena kwenye ulingo wa siasa dhidi ya chama chake cha zamani.

Lakini ni mambo yapi haswa aliyoyasema Mugabe kwenye hotuba yake?

Sikudhani kama angeweza kunigeuka'' Alisema Mugabe

Mugabe amesema kuwa Mnangagwa asingeweza kumuondoa madarakani kwani ni yeye ndiye aliyemuweka serikalini, alimsaidia alipokuwa gerezani, na hakuwaza kuwa siku moja Mnangagwa angemtoa madarakani.

0 comments: