Sunday 25 February 2018

Mkuu wa majeshi ya Korea Kaskazini azuru Korea Kusini

Ujumbe wa Korea Kaskazini unaoongozwa na jenerali wa jeshi mwenye utata umevuka na kuingia Korea Kusini kwa sherehe za kufungwa mashindano ya olimpiki ya msimu wa baridi huko Pyeongchang.

Jenerali Kim Yong-chol analaumiwa kwa kuzamisha meli ya vita ya Korea Kusini mwaka 2010 ambapo wanajeshi 46 waliuawa. Korea Kaskazini inakana kuhusika.

Familia za waathiriwa na wabunge kadhaa wa Korea Kusini walifanya maandamano wakijaribu kuzuia ziara hiyo kwenye mpaka.

Ziara hiyo inafanyika wakati kuna kuboreka kwa uhusiano kati ya Korea hizo mbili, Wakati wa mashindano ya olimpiki Korea Kaskazini na Kusini walitembea pamoja chini ya bendera moja wakati wa sherehe za ufunguzi na baadaye wakawa na kikosi cha pamoja na wanawake wa timu ya magongo.

Hata hivyo wataalamu wanaonya kuwa yanayofanaika sasa hayamalizi kikomo misukosuko ya kieneo hasa kufuatia majaribio ya nyuklia na ya makombora yanayofanywa na Korea Kaskazini.

Ujumbe wa Marekani kwenye mashindano hayo unaojumuisha binti wa rais Donald Trump Ivanka, umekana kukutana na maafisa wa Korea Kaskazini.

Siku ya Ijumaa Marekani ilitangaza awamu mpya ya vikwazo dhidi ya korea Kaskazini, Rasi ya Korea imegawanyika tangu vita vya miaka 1950 na pande zote mbili hazijawai kuwa na makubaliano ya mkataba wowote.

0 comments: