Sunday 25 February 2018

Van Gaal kuchukua mikoba ya Antonio Conte?

Kocha wa zamani wa Manchester United, Mholanzi, Luois van Gaal, anatajwa kuwa anaweza akachukua mikoba ya Antonio Conte anayeinoa Chelsea kwa sasa.

Conte amekuwa hapewi nafasi kubwa ya kuendelea kukinoa kikosi hicho licha ya kutwaa ubingwa wa Ligi msimu uliopita.

Kwa mujibu wa jarida la Mirror, linaeleza kuwa Van Gaal anapewa nafasi hiyo, na kama mazungumzo yatakuwa sawa anaweza akatua darajani kufundisha Chelsea.

Conte amekuwa akilalamikiwa na mashabiki wa Chelsea tangu achukue ubingwa wa ligi, huku wengi wakimtuhumu kwanini alimuacha Diego Costa.

0 comments: