Monday, 19 March 2018
Saturday, 17 March 2018
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mh. Paul Makonda amefunguka na kuwaomba msamaha baadhi ya wananchi ambao ameshindwa kutimiza ndoto zake na kusema anaamini ataendelea kuwatumikia na kujitahidi kuweza kugusa maisha ya kila mmoja.
Paul Makonda amesema hayo siku mbili baada ya kutimiza miaka miwili toka ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kusema kuwa ndani ya miaka miwili akiwepo madarakani anaamini amegusa maisha ya watu kwa kutumia kipaji chake, uwezo wake wote.
"Asante Mungu kwa neema zako, kama usingekuwa upande wangu na Dunia iseme sasa. Nawashukuru sana sana watumishi wenzangu Kwa kunivumilia na kunielewa katika kutimiza majukumu yangu. Zaidi nawashukuru sana wananchi naimani nimejitahidi kuwatumikia Kwa moyo wangu wote na vipaji vyote na pale niliposhindwa kutimiza ndoto yenu mnisamee"
Makonda aliendelea kufafanua na kutoa ahadi yake kwa wananchi kuwa
"Zaidi nawaahidi nitaendelea kujituma zaidi ili niyaguse maisha ya kila mmoja wetu kama ambavyo Serikali ya awamu ya 5 inavyokusudia. Mwisho si kwa umuhimu ni Kwa wadau wa maendeleo naomba mfahamu kila cent mliyoitowa ina thamani kwangu na kwa wananchi wangu. Tumefanya Mambo mengi na hakika na tumegusa na hata kuleta faraja Katika maisha ya Watu wengi. Kwakutambua mchango wenu ninaandaa siku ya kuwatambua na kuwatunuku tuzo kama asante yangu kwenu"
Machi 13, 2016 Paul Makonda aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Paul Makonda amesema hayo siku mbili baada ya kutimiza miaka miwili toka ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kusema kuwa ndani ya miaka miwili akiwepo madarakani anaamini amegusa maisha ya watu kwa kutumia kipaji chake, uwezo wake wote.
"Asante Mungu kwa neema zako, kama usingekuwa upande wangu na Dunia iseme sasa. Nawashukuru sana sana watumishi wenzangu Kwa kunivumilia na kunielewa katika kutimiza majukumu yangu. Zaidi nawashukuru sana wananchi naimani nimejitahidi kuwatumikia Kwa moyo wangu wote na vipaji vyote na pale niliposhindwa kutimiza ndoto yenu mnisamee"
Makonda aliendelea kufafanua na kutoa ahadi yake kwa wananchi kuwa
"Zaidi nawaahidi nitaendelea kujituma zaidi ili niyaguse maisha ya kila mmoja wetu kama ambavyo Serikali ya awamu ya 5 inavyokusudia. Mwisho si kwa umuhimu ni Kwa wadau wa maendeleo naomba mfahamu kila cent mliyoitowa ina thamani kwangu na kwa wananchi wangu. Tumefanya Mambo mengi na hakika na tumegusa na hata kuleta faraja Katika maisha ya Watu wengi. Kwakutambua mchango wenu ninaandaa siku ya kuwatambua na kuwatunuku tuzo kama asante yangu kwenu"
Machi 13, 2016 Paul Makonda aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Ni Simanzi na Majonzi Ibada ya Mazishi ya Mmiliki wa Mabasi ya Super Sami Aliyeuawa na Kutupwa Mtoni
Vilio, simanzi na majonzi vimetawala kwa waombolezaji kutoka jijini Mwanza na maeneo jirani wanaendelea na ibada ya mazishi ya mfanyabiashara Samson Josia yanayofanyika nyumbani kwake mtaa wa majengo mapya wilaya ya Magu mkoani Mwanza.
Mwili wa mfanyabiashara huyo uliokutwa ukiwa umefungwa kwenye viroba ukielea ndani ya Mto Ndabaka mpakani mwa wilaya za Bunda mkoa wa Mara na Busega mkoani Simiyu umewasili asubuhi ya leo Machi 16 ukitokea Hospitali ya Rufaa Mara ulikohifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi tangu juzi.
Tangu asubuhi, mamia ya waombolezaji kutoka jijini Mwanza na maeneo jirani wamekuwa wakimiminika nyumbani kwa marehemu wakitumia mabasi ya kampuni aliyokuwa akimiliki.
Mabasi ya kampuni nyingine pia yanatumika kusafirisha waombolezaji kutoka jijini Mwanza bila malipo.
Marehemu Josia aliyezaliwa mwaka 1968 alipotea tangu Februari 27 kabla ya gari lake kukutwa likiwa limeteketezwa kwa moto ndani ya eneo la hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara Machi 9.
Ibada ya mazishi inaongozwa na Mchungaji Jackson Meza kutoka Kanisa la African Inland Church of Tanzania (AICT) huku kwaya ya kanisa ambayo marehemu alikuwa mfadhili wake ikiimba nyimbo za maombolezo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Jaffari Mohamed, watu wanne wanashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano kuhusiana na kifo hicho kilichoibua hofu na maswali yasiyo na majibu miongoni mwa ndugu, jamaa, marafiki na wakazi wa jiji la Mwanza ambako marehemu alikuwa akiendesha shughuli zake za kibiashara.
Chama cha National Patriotic Front, NPF, kilichoundwa na waliokuwa mawaziri wa Zanu PF kimemtangaza Rais wake.
Chama hicho kipya kimetangaza kuwa Brigedia mstaafu Ambrose Mutinhiri atakuwa Rais wake, hatua ambayo inaelezwa kuungwa mkono na Robert Mugabe.
Ijumaa juma lililopita, Mutinhiri alijiuzulu ubunge na ndani ya Zanu PF, akionyesha kutounga mkono kuondolewa kwa Mugabe madarakani.
Mkutano wa Mugabe wa kwanza na waandishi wa habari tangu aondoke madarakani inasemekana uliandaliwa na chama cha NPF ambacho kina matumaini ya kumuondoa
Mnangagwa kwenye kinyang'anyiro cha mwezi Agosti.
Kwa miezi kadhaa sasa imekuwa ikidhaniwa kuwa huenda Mugabe atarejea tena kwenye ulingo wa siasa dhidi ya chama chake cha zamani.
Lakini ni mambo yapi haswa aliyoyasema Mugabe kwenye hotuba yake?
Sikudhani kama angeweza kunigeuka'' Alisema Mugabe
Mugabe amesema kuwa Mnangagwa asingeweza kumuondoa madarakani kwani ni yeye ndiye aliyemuweka serikalini, alimsaidia alipokuwa gerezani, na hakuwaza kuwa siku moja Mnangagwa angemtoa madarakani.






















































