Tuesday 10 April 2018

UJUE UMUHIMU WA KUNYWA MAJI MENGI KILA SIKU



Unashauriwa kunywa maji zaidi lita 2 hadi 5 kila siku ili kuepuka mawe kutengenezeka kwenye figo zako. Maji ndio husafisha seli na kuondoa sumu na kemikali zinazojitengeneza mwilini kuwa mawe.

Wanawake ndio waathirika wakubwa wa tatizo hili maana miili yao ina joto kubwa hivyo maji hukaushwa kwenye figo na mawe haya hutengenezeka kirahisi wasipokunywa maji ya kutosha.

Magonjwa ya figo yanakadiriwa kuwaathiri takribani wanawake milioni 195 duniani kote na yanashika nafasi ya 8 kama chanzo cha vifo vya wanawake duniani.

Inakadiriwa kuwa wanawake 600,000 hupoteza maisha kutokana na matatizo ya figo duniani kote kila mwaka.

Nakutakia mazingatio katika hili
Share kwa wote uwapendao...

0 comments: